Kikao Cha Dharura Lyrics
- Genre:Bongo Flava
- Year of Release:2003
Lyrics
Kikao Cha Dharura - Professor Jay
...
Professor Jay ft. Babu Ayoub
Kikao cha Dharura
VERSE 1
Prof Jay:
Nawashukuru sana wananchi kwa kweza kunipa kura
Nashangaa nimeitwa ghafla kwenye kikao cha dharula
Kikao kinaashiria kina maswali juu yangu
Hii inatokana na ndiyo mzee na ahadi zangu..
Naona watu ni wengi wananchi walio na maana
Najaribu kutafakari ni nini kinawachanganya!!
Nipo tayari kujibu maswali yenu zamu kwa zamu
Watakao uliza maswali na ningependa niwafahamu
Swali:
..Naitwa sajent Byemero kwa niaba ya jeshi la polisi
Nilikuwa nauliza zile helikopta zetu vipi?
Jibu:
Prof Jay:
Nafikiria kwanza kuanzisha chuo cha marubani
Vinginevyo mtapata ajali nyingi sana angani.
Baskeli hamjui kuendesha helikopta mtaendeshaje
Kila mtu aendeshe yake huko angani itakuwaje?
Swali:
Mheshimiwa sisi wakulima ulituahidi matrekta
Na siku zinayoyoma tu mbona haujayaleta ?
Jibu:
Prof Jay:
Wakulima mngeendelea tu kutumia jembe la mkono
Serikali haina hela bajeti imefika kikomo
Naona kilimo cha mkono kiniendelea vizuri
Jamani kazeni mikono endeleeni kukaza misuli
KIITIKIO
Wananchi tupo pamoja hapo. (siyo mzeeeeeee)
Watanzania tunaerewana kule, (siyo mzeeeeeee)
Washika dau na wapiga kura pale (siyo mzeeeeeee)
Eeehh: siyo mzee....eti, (siyo mzeeeeeee)
Wakulima tupo pamoja pale, (siyo mzeeeeeee)
Wanafunzi tunaelewana kule, (siyo mzeeeeeee)
Mabahamedi na mapolisi pale (siyo mzeeeeeee)
VERSE 2
Prof Jay:
Mabaaamedi ondoeni hofu kilio chenu nimekisikia
Ma benzi yenu yapo bandarini tayari yameshawadia
Nimemchagua kiranja ili anipe idadi yenu
Niwape funguo zenu muondoke na magari yenu.
Swali:
Ulituahidi utatujengea barabara tano tano juu na chini
Hizo zote hatutaki tunataka moja tu ardhini
Kila siku tunapita barabara zinakuwa mbaya
Umeyafumbia macho mheshimiwa huoni haya?
Jibu:
Prof Jay:
Barabara ya makwekwe nimesha imwaga kifusi
Baada ya wiki mbili itakuwa safi kama urusi
Makandarasi wanafanya kazi kutoka china na madagascar
Kuhusu vibarabara naomba muondoe shaka.
Swali:
Eeh vipi mzee mabomba kutoa maji na maziwa nchi nzima ?
Jibu:
Prof Jay:
Jamani naomba muulize maswali ya utu uzima
Mabomba kutoa maji na maziwa haiwezekani
Mlinukuu vibaya nasisitiza haiwezekani
Swali:
Mzee hali ni mbaya si tungegawana vya kwako?
Kwenye kampeni zako si ilikuwa moja ya ahadi zako ?
Jibu:
Prof Jay:
Eeehh? kugawana vya kwangu hilo swala litakuwa gumu
Familia itanitazama ebo? nina majukumu
Imeandikwa kila mtu atabeba msalaba wake
Kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake
Mbona mnaniuliza maswali mengi kunikomoa
Jamani watanzania tunajenga tunabomoa
RUDIA KIITIKIO x2
VERSE :3
Prof Jay:
Wafanyakazi wa serikalini sasa nyinyi magari ya nini?
Daladala chungu mzima mnaweza kuwahi kazini
Nasema mnapenda sana starehe kuliko kazi
Na hiyo ndio sababu mnaharibu hiki kizazi.
Wanafunzi niliwahidi mtafanyia practical mwezini
Kabla ya kupeleka mi nilifanya utafiti
Nimengundua huko mwezini kweli kuna baridi sana
Na pia kunavitisho kuwepo kambi za osama
Mkinichngua tena mtakwenda huko mapema
Nanita tekeleza kila neno ninalo sema
Sema nimesongwa na haka kamuda
Mkiniongezea muda kila kitu babu kubwa
Wengine kimya na maswali yamepungua
Yeyote mwenye swali ningependa kumtambua.
Naona mnanong'ona na wengi mmekunja sura
Hii inaonyesha mmeridhika kunipa kura
Nadhani ndugu zangu tuko pamoja...... (aagh wapi)
Jamani tupunguzeni jazba basi kidogo...... (hatutaki)
Sasa watanzania mbona mnaazisha vurugu
Nadhani mmesahau watanzania wote ni ndugu
Babu Ayoub:
Eeeh? jamani nasema hivi kikao kimeahirishwa
Jamani maafande..... Afande miraj.... Afande mzafalu,
afande nani Gondwe njooni mtusaidie huku.