![Mabawa](https://source.boomplaymusic.com/group1/M00/3D/39/rBEeMVlL-Z-AKFHgAACNtesdbBU058.jpg)
Mabawa Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2010
Lyrics
Mabawa - Migori Choir
...
Ningekuwa na mabawa, ningeruka hadi mbinguni
Ningekuwa na ufunguo, ningefungua mlango wako
{ Niingie nyumbani mwako, nikuimbie Mungu wangu
Katika makao yako, makao ya milele } *2
Malaika wanakuimbia nyimbo nzuri za furaha.
Makerubi hata maserafi wanasifu jina lako
Ningekuwa mimi ni bahari ningevuma kwa sauti
Ningekuwa mimi ni kengele ningelia usikie
Bwana mimi nitakuimbia siku za maisha yangu
Nitaimba sifa zako Bwana ili watu wasikie
Naamini kwamba siku moja nitafika mbele zako
Natamani sana kuja kwako kwenye raha ya milele