Loading...

Download
  • Genre:Bongo Flava
  • Year of Release:2021

Lyrics

Nimwage Radhi - Mrisho Mpoto

...

Instruments

Alili liliii

Furaha isiyo kifani

Kumpata mwandani

hakika wamependeza

goma lipo uwanjani

kaibiwa nani

sa unaachaje kucheza...!


Ama kweli harusi imefana tena ya kihistoria

pande zote! baba na mama naona wanashangilia

ila sitaki kuwa mnafiki jumba bovu kuniangukia

nina langu la moyoni

ningependa kuwaambia

Bi harusi mashoga wa kupupia hao ni wa kuwangalia

wako wale wa hali gahn...wanakuja kuchungulia uwaombe samahani uwakomeshe wambea,

eti wifi umepika nini na mimi utanigaia?

waambie wapika dagaa wenye pilipili nyingi zinakutosha wew na mume wako,

wako wao watakimbia.


Eeeh....!

Aiiih shemeji chukua ya mumeo

usiskize ya fulani

Na hii ndio meseji sema na mumeo usifuate ya jirani

kwa furaha niliyo nayo niacheni nimwage radhi

alilililiiiih,

mi nataka nimwage radhi,

Aiyoyo niacheni nimwage radhi

mi nataka nimwage radhi! alilililiiiih


Ng'ombe anapoita ndama tunasema kuwa analia,

kupigwa na kulalama hatujawahi kuskia

hakika mmependeza

ninavyomfahamu bi harusi sipati kusimulia

nimetokea ruvuma,mchomoro namtumbo lindi mtwara mpaka chitohori nimezisikia

sifa za binti huyu molaa amemjalia

binti hapendi majungu hakika nachowaambia ukimuazima viatu na gauni anakuachia

Bwana harusi tunakupa mke ukaishi naye vyema nyumbani

huna kitu usimfiche mwambie taabani

ikiwezekana mkakope mkono uende kinywani

usimpige mateke

kisingizio kitu fulani

oooh umefanya nini jana hakuliki leo ndani

mtoto bado mteke usimkomaze kwa ngumi

ukimshindwa mrudishe kwao hajaua huyu

Mumeo akienda kazini

akirudi salimia

wala usikae chini chakula kumsukumia

mkaribishe ndani hali ukimjulia

muulize za kazini kwa tabasam murua

kisha msindikize bafuni hata kama anapajua

Alafu wew tafuta kiti jikoni kimbilia

Chukua simu yako meseji ukimtumia

mwambie

Asilani bila wewe chakula hakitaingia


Eeeh....!

Aiiih shemeji chukua ya mumeo,

usiskize ya fulani,

na hii ndio meseji

sema na mumeo usifuate ya jirani

kwa furaha niliyo nayo

Niacheni nimwage radhi

alilililiiiih

mi nataka nimwage radhi,

Aiyoyo niacheni nimwage radhi,

mi nataka nimwage radhi!

alilililiiiih

Nawaomba niishie hapa

taharishi huwa hafungwi

Naomba nichape lapa

yaliyobaki ni ya makungwi

niliowakera samahani

kusema ni jukumu langu

nawaomba muishe kwa amani

hiyo ni furaha yangu


mmmmh

ndoa ni kama safari

tuombe yake dua

atuepushe na shari

saa chini ya jua

Ah somo yake mwali

Ainuke

Mama yake mwali

Ainuke

Baba yake mwali

Ainuke

Aje kati tulicheze goma

Ah mama yake mwali

Ainuke

Dada yake mwali

Ainuke

Shangazi yake mwali

Ainuke

Aje kati tulicheze goma


Niacheni Nimwage radhi

Mi nataka tumwage radhi

Niacheni Nimwage radhi

Mi nataka tumwage radhi


lyrics by NjauMsafiri

Similar Songs

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234
          -You can log in via below methods-
          Reset password via e-mail
          -or-
          Reset password via e-mail
          Feedback on resetting password
          * It may take a longer time

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status