
Sitasumbuka (Wokovu 50) Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2024
Lyrics
Sitasumbuka kwa kuwa Mungu ananitunza daima, anachukuwa mizigo yangu nyakati zote za mwendo.
Sijaiona nyingine siku, na jana imetoweka, na leo Mungu anazijuwa hitaji zote ninazo.
Sitasumbuka kwa kuwa Mungu ni baba yangu kabisa. Hawezi kunisahau mimi ingawa akijificha.
Sijaiona nyingine siku, na jana imetoweka, na leo Mungu anazijuwa hitaji zote ninazo.
Sitasumbuka kwa kuwa Mungu anishibisha neema, anipa yote yanifaayo kwa roho yangu na mwili.
Sijaiona nyingine siku, na jana imetoweka, na leo Mungu anazijuwa hitaji zote ninazo.
Mauwa yote anayavika, Na ndege wote wa anga wanapokea chakula chao pasipo shamba na ghala.
Sijaiona nyingine siku, na jana imetoweka, na leo Mungu anazijuwa hitaji zote ninazo.
Ninafurahi katika Bwana, Na kama ndege naimba. Najuwa kwamba nyakati zote babangu ananitunza.
Sijaiona nyingine siku, na jana imetoweka, na leo Mungu anazijuwa hitaji zote ninazo.