Loading...

Download
  • Genre:Spoken Word
  • Year of Release:2023

Lyrics

Tulipofika ni mbali

Itisha madafu utulize akili

Keti chini nikusimulie hadithi za Misambwa

Na Masinde wa Nameme ohkwa Mwasame

Godpapa wa dini ya Musambwa


Babu aliniambia alikuwa msumbufu kweli

Sijui kama walijuana

Lakini najua alileta shida sana hata baada ya kifo

Kabla ya kuaga, unajua alifanya nini?


Sikiza

Aliagiza mti wa mkuyu utolewe na mizizi yake

Ili kuipa njia kaburi lake

Familia nayo iliamua kupuuzia mbali na kumzika kwingine

Lakini

Shaka

Walipata kaburi la mtu mwengine

Katika ile sehemu waliyojichagulia wenyewe

Mwishowe alizikwa kama alivyoagiza mwanzoni


Anyway, alikuulizia mama

Najua anakuenzi

Nilimwelezea unavyoipa pumzi yangu maana

Ninavyokupenda zaidi ya mapenzi na mapeni

Nilimwambia asianze haraka za harusi au wajukuu

Najua tayari keshaanza kutenga visenti vya kuku na zawadi za leso


Tukifika kule vumilia

Usidanganywe na tabasamu za majirani

Watakumeza mzima mzima

Salamu ziwe za hewani kama za Corona

Waambie unaumwa na tumbo so huwezi kula chochote

Najua tunatofautiana kimila na safari hii si ya wengi

Yamesemwa mengi sana juu yako na wenye akili ndogo lakini usi-mind

Those are just stereotypes that entertain narrow minds

I'd fall for the hills of Murang'a again if I had to do it nine thousand times

A thousand for each daughter of Mumbi


Tafadhali wavumilie mama na baba

They grew up under those dividing myths lakini

Wanajitahidi kukuchukua kama binti yao

Ipe muda


Dada zangu wakiongea kwa lugha ya mama usichukulie vibaya

Haupo kwenye maongezi yao

Najua kidogo itawauma kujua kaka yao wa kipekee

Karibuni atakuwa na familia mpya

Lakini niamini

Wewe ni familia yao pia

Usiskize ya watu

Barabara tulizopitia hawazifahamu

They don't know what it took for us to smile

They didn't see us crawling to this place

Hawakuona machozi yetu juu walikuwa busy na rangi ya lipstick kwa mdomo

Na eyebrows zilivyochongwa

Tukimeza bitter saliva walidhani ni utamu wa maisha tuna-sample

Hawakuona ilivyokuwa ngumu ku-swallow

Walituandalia meza wakasahau viti ndiyo watukalie

Si unajua binadamu ana roho ngumu

Yasikutishie hayo


Nipe mkono wako

Nitakuwa shujaa wako

Nitakufariji

Nitakulinda

Wacha upinde wa mvua na furaha ukumbatie moyo wako

Jua lichore tabasamu usoni na mawingu ya uwoga yapotee

Safari ya mbali huanza na hatua na mbugani ushatua

Jihisi nyumbani ukiwa nami

+

      -   or   -

      -   or   -

      NG +234
          -You can log in via below methods-
          Reset password via e-mail
          -or-
          Reset password via e-mail
          If you have any questions, please feedback on Boomplay App or send an email to [email protected].

          Please Select A Playlist

          Add New Playlist

          Share on

          Embed: Love & Light EP

          Custom Size :

          • Default
          • Desktop(300*600)
          • Mobile(300*250)

          Type :

          • HTML/HTML5 (WordPress Supported)
          Get Boomplay Premium
          for
          Payment Method
          Pay With
            Review and pay
            Order Date
            Payment Method
            Due Today
            Flutterwave
              Subscription Successful

              Congratulations! You have successfully activated Boomplay 1 Month Premium.

              Now you have access to all the features of Boomplay App.
              Payment Failed

              Please check your balance and then try again.

              You'll lose your subscription if we don't have a working payment method for your account, so please check your payment details.
              Need help? Contact Boomplay Subscription Support.
              Payment Processing...
              10 s

              Payment is being processed by . Please wait while the order is being comfirmed.

              Payment Processing
              Your order is processing, and it may take up to a few days for the service provider to handle your payment. Please kindly stay tuned and check your order status in ‘User Center’.
              About Order Status